Malumbano hayana maana tuyaepukeni.


Related imageWaislamu nchini wametakiwa kuacha malumbano na kuingizana kwenye kufru kwa kisingizio cha madhehebu nabadala yake kuwakitu kimoja ili kuusongesha mbele uislam.

Nasaha hizo zimetolewa na Shk Khalfan bin Suleiman Khalfan wakati akifungua msikiti uliopo mkungu malofa chake chake kwaniamba ya Mufti mkuu wa Zanzibar Shkh Saleh Qabi.

Amesema vitendo vya baadhi ya waumini kuwashajiishisha wengine kupinga madhehebu yaw engine nijambo linalo kinzana na maamrisho ya Allah (Sw).

Aidha amesema nimuda sasa kwa waislam kuwakitu kimoja ili kuweza kuzitekeleza ibada zote kwa ukamilifu pasipo namalumbano.

Hatahivyo amewataka wafanya biashara kuiga juhudu zilizochukuliwa katika kufanikisha mskiti huwo hadi kukamilika kwake ili iweze kutoa nguvu kwa waumini kuweza kuzitekeleza ibada katika mazingira yaliobora.

Akitoa neno la shukurani kwa wafadhili walio jenga mskiti huwo Shkh Zahor Saleh Omar amesema nijambo lafaraja kuwekeza kwa Allah (SW) kwani malipo yake hayaishii duniyani pekee nahata akhera pia malipo yake atayakuta yoyote atakae fanya jambo jema.

Amesema miskiti ni nyumba za Mwenyezimungu hivyo tunatakiwa kuilinda kwa halizote ili kuweza kuinusuru dini ya Allah (SW) dhidi ya maadui wasio ipendelea mema uislam.

Zaidi ya milioni 300 zimetumika katika ujenzi wa msikiti huwo hadi kukamilika kwake ambao umejengwa kwa ufadhili wa Shkh Ahmed Nassor .

Comments