Alisema hayo wakati akifungua mkutano wa kitaifa wa kujadili kusinyaa kwa nafasi za asasi za kiraia na vyombo vya habari uliofanyika hoteli ya Ocean View Kilimani.
Alisema hatua hiyo itasaidia kuondosha tatizo la kusinyaa kwa uhuru
wa vyombo vya habari ambalo kwa sasa limekuwa likijitokeza dunia nzima.
Aidha alisema vyombo vya habari vina umuhimu na nafasi kubwa kwa
taifa kutokana na mchango wao hususan katika kusukuma masuala ya
maendeleo na jambo la msingi ni ushirikiano kwenye maeneo ya kazi ili
kuleta tija ya uwajibikaji.
Nae Kiondo Reubet Mshana, alisema waandishi wa habari wanapaswa
kujilaumu wenyewe kutokana na mwenendo wao ambao mara kadhaa umekuwa
ukikiuka maadili na taratibu zao za kazi.
Kuhusu kufungwa kwa baadhi ya vyombo vya habari, alisema unatokana na
ukosefu wa taarifa sahihi ambazo zimekosa uchunguzi na vielelezo vyenye
ushahidi wakati wanapoandika habari.
Alisema, mwandishi wa habari lazima ajikubalishe kujituma kwa
weledi,ufasaha kwa kufuata maadili ya kazi yake na sio kujenga tabia ya
kuilaumu serikali kwa mambo yasio na msingi.
Mwanasheria Hardlod Sungusia, alisema katiba za Zanzibar na Tanzania zimeeleza umuhimu wa wananchi kupata habari huku maadili na taaribu kwa vyombo vya habari zikihimiza umuhimu wa uhuru, haki na kuzingatia utawala wa sheria.
Zanzibarleo.
Comments