Alisema hayo wakati akiaghirisha mkutano wa 11 wa Baraza la tisa la wawakilishi, Chukwani Wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja.
Hivyo aliwataka wananchi wanaomiliki vyombo vya usafiri kufuata
sheria za usalama wa abiria ili kunusuru maisha ya wananchi na mali zao.
Alisema serikali itaendelea kusimamia sheria za usalama wa vyombo vya
usafiri wa majini na nchi kavu bila ya kumuonea muhali mtu yeyote.
Aidha kwa mara nyengine aliwaomba wananchi wanaoishi maeneo hatarishi
kuondoka katika maeneo hayo, ili kuondoa uwezekano wa kutokea maafa
yanayoweza kutokea.
Kuhusu udhalilishaji, alisema jamii inayowadhalilisha wanawake na
watoto, haiwezi kupata maendeleo ya haraka na hukosa thamani na heshima
mbele ya macho ya jamii nyengine.
Alisema ni jambo la kushangaza kuona baadhi ya akina baba wanaacha
jukumu lao la malezi na badala yake kujiingiza katika kundi la
wadhalilishaji wa watoto wa damu au wale wanaowalea.
Alisema vitendo hivyo ni vya kinyama na vya aibu kwa jamii yenye kufuata mila, desturi, silka na utamaduni.
Hivyo aliwaomba wazee wenye hulka kama hiyo wabadilike ili kuwapa
faraja watoto wao wanaopaswa kupata furaha na amani katika maisha yao ya
kila siku.
Alitanabahisha kwamba ulezi wa zamani wa kuwaacha watoto peke yao
nyumbani umepitwa na wakati kwani unatoa fursa kwa wahalifu kuitumia
nafasi kama hiyo kutekeleza vitendo vyao viovu.
Zanzibarleo.
Comments