Ndege hiyo iliyopangiwa safari nambari JT-610 ilikuwa inakwenda Pangkal Pinang, jiji linalopatikana katika visiwa vya Bangka Belitung. IIitoweka kutoka kwenye mitambo ya rada saa kadha baada ya kupaa, ilipokuwa inavuka bahari.
Katika kikao na wanahabari, maofisa walisema ndege hiyo ilikuwa imewabeba abiria 178 watu wazima, watoto watatu, marubani wawili na wahudumu watano.
Msemaji wa shirika la uokoaji na kutafuta manusuera, Yusuf Latif aliwaambia wanahabari: "Imethibitishwa kwamba ndege hiyo imeanguka."
Comments