Waziri Mkuu Aunda Tume ya Watu 7 Kuchunguza Chanzo cha Ajali ya MV Nyerere.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameunda Tume ya watu 7 kuchunguza ajali ya MV Nyerere ikiongozwa na Jenerali Mstaafu, George Waitara na Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi

Pia amesema Rais Magufuli  ameagiza kuitishwa kwa zabuni ya kutengeneza kivuko kipya cha uzito wa zaidi ya tani 50 na uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 200 ili kichukue nafasi ya Mv Nyerere wakati kikiendelea na matengenezo. 

Comments