SERIKALI
kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
imesisitiza kuwa huduma za uzazi kwa wajawazito zinatolewa bila ya
malipo katima Hospitali na vituo vya afya vya Serikali.
Hayo
yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa ziara yake ya kujua hali ya
utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Rufaa Temeke, Amana na
Mwananyamala leo jijini Dar es salaam.
“Nimesikia
pale wajawazito wameniambia wamekuja na vifaa vya kujifungulia kutoka
majumbani mwao sitaki kusikia mwanamke mjamzito analipishwa wala kuja
vifaa vya kujifungulia kwani sera yetu inasema huduma za uzazi ni bure”
alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha
Dkt. Ndugulile alisema kuwa wanawake wajawazito , watoto chini ya miaka
5 na wazee wasio na uwezo wanapata matibabu bure kulingana na sera ya
Afya inavyosema. Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa kila mtoa
huduma anapaswa kuandika taarifa ya mgonjwa kabla na baada ya kumpa
huduma katika kituo chake cha kazi.Aidha Dkt. Ndugulile aliwataka watoa
dawa katika hospitali na vituo vya afya kuandika majina asilia ya dawa
na siyo yale ya kampuni pamoja na kufuata muongozo wa dawa uliyowekwa na
Serikali.
“Marufuku
watoa dawa kuwaandikia wagonjwa dawa na kwenda kununua nje ya kituo cha
afya na badala yake dawa zote zitolewe katika hospitali au kituo cha
afya kama zimeisha zinatakiwa kuagizwa kwa haraka na nauagiza uongozi wa
Hospitali ya Amana kuwarudishia wagonjwa wa wodi ya watoto waliokwenda
kununua dawa nje leo hii ” alisema Dkt. Ndugulile.
Kwa
upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Temeke Dkt. Amaan
Malima amesema kuwa changamoto kubwa inayowakumba ni upungufu wa
watumishi .
Naye
Mkurugenzi Msaidizi wa Hospitali ya Rufaa ya Amana Dkt. Meshack
Shimwela amesema kuwa anaomba radhi kwa tatizo hilo lililojitokeza kwani
hakuna tabia kama hiyo hospitalini hapo na amehaidi kulifanyia kazi
haraka iwezekanavyo.
Mpekuzi.
Comments