WAZIRI
wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa, jana Julai 5, 2018
ametembelea mradi wa uboreshaji wa mfumo wa usambazaji maji Dar es
Salaam na Pwani ambao umefikia asilimia 87.5 kukamilika na kumuhimiza
mkandarasi kumalizia asilimia iliyobaki kwa wakati vinginevyo atachukua
hatua kali.
Profesa
Mbarawa amesema, mradi huo ambao unatekelezwa na Serikali kupitia
Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA), unathamani ya shilingi
bilioni 72.43 na ni mradi muhimu sana katika utoaji huduma kwa wananchi.
“Mkandarasi
yuko kwenye site lakini kasi yake hairidhishi, hivyo sisi kama serikali
tunajaribu kutatua kero hii ya maji kwa wananchi, lakini mkandarasi
kidogo analeta shida, kama mjuavyo mradi ulianza mwaka 2016 mwezi Machi
na ulitarajiwa kukamilika Novemba 2017 utaona tuko nyuma karibu miezi
18.” Amesema
“Kwanza
tunataka uwepo kwenye site saa 24, na sio tunakuona tu lakini tuone
unafanya kazi, pili ukishinbdwa kumaliza mradi huu kama tulivyokubaliana
mwezi Septemba uelewe kwamba hii ndio itakuwa mara yako ya mwanzo na ya
mwisho kupata kazi tena hapa Tanzania, na tatu tutakutoa kwenye usajili
wa chama cha makandarasi yaani bodi ya makandarasi na hii maana yake
hutaweza kufanya kazi tena hapa Tanzania na mwisho tutachukua Pasipoti
yako ya kusafiria ili kuhakikisha kwamba unafanya kazi na unamaliza.”
Alisema.
Ziara
hiyo ya Profesa Mbarawa imemuwezsha kujionea maendeleo ya utekelezaji
wa mradi huo ulioanza Machi 2016 na unaohusisha ujenzi wa matenki matano
(5) ya kuhifadhi na kusambaza maji yenye ukubwa wa kuhifadhi lita
milioni 5.0 hadi 6.0.
Pia
alitembelea ujenzi wa vituo vine (4) vya kusukuma maji vilivyo na
matenki yenye uwezo wa kuhifadhi lita milioni 3.0 kila moja, ununuzi na
ufungaji wa pampu kubwa 16 za kusukuma maji ununuzi wa transfoma na
ufungaji wa njia za umeme wa msongo mkubwa, ununuzi na ulazaji wa
mabomba makubwa ya ugawaji maji na ulazajiwa mabomba ya usambazaji maji
mitaani yatakayokuwa na urefu wa jumla ya kilomita zipatazo 477.
Kwa
mujibu wa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Dkt. Suphiani Masasi,
mradi huo utanufaisha maeneoya Salasala, Bunju, Wazo, Makongo,
Changanyikeni, Bagamoyo, Mpiji, Zinga, Kiromo, Kitopeni, Ukuni, Kerege,
Buma, Mataya na ukanda maalum wa WPZA ambayo ni maeneo yanayohudumiwa na
mtambo wa Ruvu Chini.
Baadhi ya vifaa vya kukamilisha mradi huo vikiwa kwenye karakana huko Boko nje kidogo ya jiji
Aidha
mradi pia utanufaisha maeneo yaliyopo kati ya Mbezi Louis na Kiluvya
ambayo ni Kiluvya yenyewe, Kibamba, Mbezi, Msakuzi, Makabe, Malamba-
mawili na Msigani na maeneo haya yanapata maji kutoka Mtambo wa Ruvu Juu
ambao ulizinduliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania
Juni 2, 2017.
Mtendaji
Mkuu huyo wa DAWASA alimueleza Mhe. Waziri kuwa lengo la mradi ni
pamoja na kuhakikisha kuwa wananchi wa kawaida wenye viwanda na biashara
katika eneo lote la mradi wanapata huduma bora za maji hasa baada ya
maji kuongezeka kufuatia kukamilika kwa kazi za upanuzi wa mitambo ya
maji Ruvu Juu na Ruvu Chini.
Mpekuzi.
Comments