Akiwasilisha
matokeo ya utafiti uliofanywa kupitia Mradi wa PartoMa Daktari wa Wodi
ya Wazazi wa Hospitali hiyo Dk. Natasha Housseine, alisema pamoja na
juhudi kubwa zinazochukuliwa na madaktari na wakunga, mapungufu hayo
yanasababisha baadhi ya wakati watoto kupoteza maisha muda mfupi baada
ya kuzaliwa kwa kukosa uangalizi mzuri.
Dt. Natasha alisema
Hospitali ya Mnazimmoja wastani ya watoto wachanga 12000 huzaliwa kwa
mwaka idadi ambayo ni kubwa ukilinganisha na nyenzo na wafanyakazi
waliopo ndani ya wodi.
Alieleza
kuwa kutokana na tatizo hilo, Mradi wa PartoMa ambao unalenga kufuata
taratibu zote za kumuangalia mama mjamzito tokea mwanzo wa kupata
uchungu hadi kujifungua umeanzishwa miaka mitatu iliyopita katika
Hospitali hiyo.
Alisema
Mradi wa PartoMa unaotekelezwa kwa pamoja na Hospitali Kuu ya
Mnazimmoja na Chuo Kikuu cha Copenhagen unasaidia kutoa miongozo na
mafunzo kwa madaktari na wakunga wachanga ili kuhakikisha usalama wa
wazazi wakati wa kujifungua na watoto wachanga baada ya kuzaliwa.
Daktari
bingwa wa magonjwa ya wanawake na watoto wachanga wa Hospitali Kuu ya
Mnazimmoja ,Dk. Salma Abdi Mahmoud, alisema Wizara ya Afya imekuwa
ikifanyakazi kwa ushirikiano mkubwa na madaktari wa Zanzibar, kutoka nje
ya nchi na Taasisi za Kimataifa kuhakikisha mama wajawazito na watoto
wachanga wanapatiwa huduma bora wakati wa kujifungua na baada ya
kujifungua.
Alisema
mahitaji muhimu ya mama wajawazito na watoto wachanga hivi sasa
yamesambazwa katika maeneo yote mijini na vijijini na aliwashauri
akinamama kuzitumia huduma hizo kuimarisha afya zao na watoto
wanapozaliwa.
Zanzibarleo.
Comments