Dk. Shein aliyasema hayo, ikulu mjini Zanzibar alipokutana na
uongozi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi wakati
ulipowasilisha utekelezaji wa mpango kazi wa mwaka 2017/2018 na mpango
kazi wa utekelezaji kwa mwaka 2018/2019.
Huo ulikuwa mkutano wa mwisho kwa kipindi hichi kwa utaratibu
aliojiwekea Dk. Shen wakukuna na viongozi na watendaji wa wizara
mbalimbali.
Alitoa pongezi za dhati kwa uongozi na wafanyakazi wa ofisi ya Rais
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa utendaji mzuri wa kazi zao,
hatua inayompelekea kuendelea kufanyakazi vyema za kuwatumikia wananchi.
Alieleza kuwa uwasilishwaji mzuri wa mpango kazi wa Ofisi hiyo
umetokana na uzoefu wa muda mrefu uliopatikana tangu kuanza kwa zoezi
hilo la bango kitita ambalo lilianza mara tu alipoingia madarakani.
Dk. Shein alimpongeza waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi kwa kumsaidia katika shughuli mbali
mbali za kazi na kumpongeza Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee kwa utendaji wake mzuri.
Aidha, aliwashukuru na kuwapongeza washauri wake wote kwa kuendelea
kumshauri mambo mbalimbali ya msingi na kutoa nasaha kwa uongozi wa
ofisi hiyo huku akiwataka kuwasikiliza.
“Nimeshuhudia uwezo mkubwa mlionao wafanyakazi wa Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na nimethibitisha hili kwa kufuata ule
msemo usemao ukitaka kuwajua wafanya kazi wa ikulu wape kazi”,alisema.
Zanzibarleo.
Comments