Aliyasema
hayo, Ikulu mjini Zanzibar alipokutana na uongozi wa Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais, wakati ilipowasilisha utekelezaji wa mpango kazi wa mwaka
2017/2018 na mpango kazi wa utekelezaji kwa mwaka 2018/2019.
Alitumia
fursa hiyo kumpongeza Balozi Seif kwa kumsaidia kazi pamoja na
kuupongeza uongozi wa ofisi hiyo na watendaji wake kwa kufanya kazi
zinazoonekana na zisizoonekana zikiwemo mazingira na UKIMWi.
Pia,
alimpongeza Waziri, Naibu Waziri na watendaji wengine wote wa ofisi
hiyo kwa kazi nzuri wanazoendelea kuzifanya ikiwemo katika baraza la
wawakilishi.
Pamoja
na hayo, alisisitiza haja ya usimamizi katika utekelezaji wa majukumu
ya kazi hatua ambayo huleta ufanisi mkubwa na uwajibikaji kazini.
Alieleza
kuwa kuanzishwa kwa taasisi za utafiti ambazo zimeundwa kwa mujibu wa
sheria kuna umuhimu mkubwa katika kufikia malengo yaliokwekwa juu ya
suala zima la tafiti hapa Zanzibar.
Alisisitiza
kuwa upimaji wa UKIMWI ni jambo la hiari hivyo alitoa wito kwa uongozi
huo kuendelea kutumia utamaduni wa kuwashajiisha wananchi kwenda kupima
badala ya kuwalazimisha.
Zanzibarleo.
Comments