Polisi wilayani Serengeti Mkoa wa Mara wanawashikiria watu kumi kwa kosa la kukutwa na nyara za Taifa kinyume cha sheria.
Kamanda
wa Polisi mkoa huo, Juma Ndaki akizungumza na waandishi jana Jumapili
Julai 22, 2018 alisema watuhumiwa hao wamekutwa na vipande 531 vya nyama
kavu, mikia 24 ya nyumbu, mikia 12 ya pundamilia, nyaya 75 za kutegea,
mapanga mawili, visu viwili, dumu nane za maji na baiskeli 10.
Ndaki
alisema mzigo huo ulilkamatwa kwenye kambi yao ya ujangili eneo la
Togoro ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ushirikiano wa
askari wa Hifadhi hiyo na Polisi wilayani humo.
“Watuhumiwa wote ni wakazi wa kata za Nyambureti na Nyamatare wilayani Serengeti,” alisema Ndaki
Mpekuzi.
Comments