Kiongozi mbio za mwenge akataa kufungua kituo cha afya.

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Charles Francis Kabeo amekataa kufungua mradi wa kituo cha afya cha Uroa wilaya ya Kati Unguja, kutokana na thamani ya mradi huo hailingani na kiwango cha mradi huo.

Alisema hayo huko Uroa katika ufunguzi wa mradi huo ambapo alifahamisha kwamba thamani ya mradi huo ni kubwa na hailingani na thamani ya ujenzi wa mradi na kwamba hatokifungua kituo hicho.

Mradi wa kituo cha afya Uroa wenye chumba cha kutolea huduma za mama wajawazito na watoto, chumba cha ushauri nasaha, maabara na huduma nyengine umegharimu shilingi milioni 382 hadi kumalizika kwake.

Akitoa salamu za mbio za mwenge wa uhuru kwa wananchi mbalimbali kiongozi huyo amesisitiza umuhimu wa wazazi kuwekeza katika elimu kwa maendeleo ya taifa na watoto wao.

Alifahamisha kwamba serikali zote mbili ya Zanzibar na Tanzania bara zinaendelea na jitihada zake za kuimarisha sekta ya elimu kuanzia ngazi ya msingi hadi chuo kikuu.

Zanzibarleo.

Comments