Bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kuwasilishwa leo.

bajetiWaziri wa fedha na Mipango, Dk. Khalid Salum Mohammed, leo anatarajiwa kuwasilisha bajeti ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Waziri huyo anatarajiwa kusoma bajeti hiyo, katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Mjini, ulioko Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Akitoa muelekeo wa bajeri hapo juzi, Dk. Khalid alisema serikali inakusudia kutumia shilingi trilioni 1.3, zikiwamo shilingi bilioni 807.5 zitazokuwa ni za vyanzo vya ndanina shilingi bilioni 464.2 kutoka kwa washirika wa maendeleo.

Aidha alisema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka huo wa fedha inatarajia kukua kwa uchumi wake kwa kasi ya 7.7.

Ofisa Uhusiano wa Baraza la Wawakilishi, Himidi Choko, alifahamisha kuwa tayari maandalizi ya usomaji wa bajeti hiyo yamekamilika ndani ya Baraza hilo ambapo wanatarajia kupokea wageni mbali mbali walioalikwa katika taasisi tofauti.
Zanziba24.

Comments