Waziri
wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema licha ya utajiri wa
rasilimali uliopo nchini wananchi wameendelea kuwa maskini.
Akizungumza
jana Mei 2, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa taasisi ya
utafiti wa uchumi na jamii (ESRF) Dar es salaam, Dk Mpango
aliyemwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitaja sababu kubwa kuwa ni
kutokuwepo kwa uwiano kati ya ukuaji wa uchumi na sekta ya Kilimo.
“Tanzania
ni tajiri wa rasilimali. Tunayo maziwa kama Victoria, Tanganyika,
Rukwa, Nyasa na mito mingi inayotoa fursa za uvuvi na uzalisha wa umeme.
Tuna utajiri wa madini kama dhahabu, almasi, Tanzanite, ruby, bati,
chuma, mkaa, uranium, gesi ya asili, helium na mengineyo,” alisema Dk
Mpango.
Aliongeza
kuwa Tanzania ni kituo kikubwa cha utalii ikiwa na urefu wa kilometa
1,200 za fukwe za bahari, hifadhi za wanyama, huku ikiwa nchi ya amani
na utulivu isiyokuwa na machafuko ya kikabila.
“Hata
hivyo, uporaji wa maliasili umesababisha maisha ya Watanzania walio
wengi kuwa masikini, huku wachache wakifaidi rasilimali hizo,” alisema
Dk Mpango.
Alitaja
chanzo cha matatizo hayo kuwa pamoja na ukosefu wa teknolojia ambapo
alitoa mfano wa wachimbaji wadogo wa madini wanaoshindwa kupata madini
ya kutosha kwa kutokuwa na teknolojia.
Mpekuzi.
Comments