Wakizungumza Baadhi ya
Wananchi wanaofaidika na mradi wa tassaf Mkoa wa Kaskazini Unguja Shehia
ya Mkataleni wamesema mradi wa tassaf ni wa kupigiwa mfano katika
kuinua maisha ya wanyonge kwani wameweza kuwasaidia watoto wa maskini
kuweza kusoma na wazazi kuweza kujiajiri wenyewe kupitia miradi
mbalimbali waliyoianzisha kujiajiri.
Kwaupande wake Mratibu kutoka tassaf upande
wa unguja Makame Ali Haji amesema Zanzibar zipo kaya ambazo zilikuwa
zinaishi katika mazingira magumu na hatarishi , Serikali kwa
kuliona ikaamua kwa makusudi kuwasaidia wananchi wake kuondokana na
maisha hayo.
Amesema kuwa ujio wa mradi wa tassaf kwa
kuzisaidia kaya maskini umeweza kuwainua wananchi wengi kwenye wilaya
mbalimbali za unguja na pemba na wananchi wengi wameweza kunufaika na
kuweza kujikimu kimaisha.
Kwaupande wake Sheha wa Shehia ya Mkataleni
Sharifu Ali Makame amesema zaidi ya wananchi 216 katika shehia yake
wananufaika na mradi huo wa kusaidia kaya maskini na wameweza kupiga
hatua wananchi katika nyanja za kimaendeleo.
Sheha huyo ameiyomba serikali
kuzidisha kasi ya kuwasaidia wananchi wengine ambao bado hawajaingiwa
katika mradi huo ili nao waweze kujikwamua na hali ngumu ya maisha.
Zanzibar24
Comments