Wabunge
wa CCM, Sixtus Mapunda (Mbinga Mjini) na Mussa Sima (Singida Mjini)
wameitaka Serikali kutoa majibu ya lini wafanyakazi wataongezewa
mishahara ili kuwakwamua wananchi kiuchumi.
Wabunge
hao wamehoji hayo leo Mei 2, 2018 bungeni mjini Dodoma wakati wakiomba
mwongozo wa Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge wakitumia kanuni ya 67
(8) baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu.
Mapunda
amesema; “…kwa kuwa kuondoa umaskini wa kipato, kuna uhusiano wa moja
kwa moja na ongezeko la mishahara ya watumishi wa Serikali wa pande
zote. Na kwa kuwa jana siku ya Mei Mosi Rais (John Magufuli) aliji
‘commit’ kuwa ongezeko la mishahara pamoja na mambo mengine litazingatia
hali halisi ya uchumi, uwezo wa taifa na uwezo halisi wa Serikali.”
“Na
kwa kuwa ameji ‘commit’, Serikali inatoa kauli gani lini mishahara hiyo
itapanda kwa sababu suala hili jana limeacha sintofahamu kwa wananchi,”
ameongeza:
Naye
Sima licha ya kumpongeza Rais Magufuli kwa hotuba aliyoitoa jana mjini
Iringa amesema; “Lakini kama bunge, tungetaka kujua ni lini sasa
watumishi hawa watapandishiwa mishahara.”
Akitoa majibu ya miongozo hiyo ya wabunge, Chenge amesema jana hata yeye alimsikiliza vizuri Rais Magufuli akielezea suala hilo.
Chenge amesema: “Rais alisema hali ikiwa nzuri ataongeza mshahara na ataongeza kikweli kweli. “
Mpekuzi.
Comments