
Akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari
kuhusiana na siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Ukumbi wa Wizara
ya habari Kikwajuni Mjini Zanzibar,Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya
kale Mahamoud Thabit Kombo amesema Serikali inatambua umuhimu wa vyombo
vya habari hivyo itaendelea kutoa taarifa ili kuwawezesha wananchi
kunufaika na haki zao za msingi.
Amesema wananchi wanahitaji kujua taarifa
mbalimbali kuhusiana na Nchi hivyo waandishi wa habari watakapopewa
taarifa kwa wakati wataweza kuisaidia jamii na serikali kwa ujumla.
Waziri kombo amewataka Waandishi wa habari
kuendelea kufanya kazi zao kwa kufuata Sheria na Maadili ya Kazi zao
ili kujiepusha na matatizo ambayo yaweza kuondoa amani ya Nchi.
Hata hivyo amesema Serikali haitamvumilia
Mwandishi au Chombo Chochote kitakachojihusisha na utoaji wa taarifa
ambazo zitaleta athari katika jamii ili kuwawezesha wananchi kupata haki
zao na Nchi kuendelea kubaki katika hali ya amani na Usalama.
Madhimisho ya Siku ya Vyombo vya
Habari huadhimishwa kila ifikapo may 3 ya kila mwaka ambapo kwa
Zanzibar yanatarajiwa kuadhimishwa katika Ukumbi wa Wawakilishi la
Zamani yakiwa na ujumbe usemao WAJIBU WA UONGOZI ,VYOMBO VYA HABARI HAKI NA SHERIA.
Zanzibar24.
Comments