
Akizungumza wakati wa kukabidhi boti mbili
za mwendo kasi kwa kikosi cha kuzuwiya magendo zanzibar na kikosi cha
uwokozi zanzibar ambapo boti hizo zimetolewa na taasisi ya
rom solution Inayojihusisha na masuala ya ulinzi zanzibar waziri wa nchi ofisiya rais serikali za mitaa na idara maaalum za SMZ
Haji Omari Kheri huko bandrini mjini zanzibar.
Amesema kuwasili kwa boti hizo za kisasa kutapelekea ufanisi na utekelezaji
wa majumkumu katika vikosi
vya usalama hususani masuala ya ulinzi na uwokozi katika
maeneo ya bahari.
Aidha mkuu wa mkoa mjini magharibi ayoub mohammed mahmoud amesema zanzibar
imejenga historia kwa
kupokea boti hizo hususani ya uwokozi katika mkoa wake.
Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa boti hizo wakuu
wa vikosi vya kmkmk na
zima moto wamesema kukabidhiwa kwa boti hizo kutajengea uwezo kwa watendaji wa taasisi zao kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuondosha changamoto zinazowakabili katika masuala ya ulinzui na uwokozi.
Makabidhiano ya boti hizo yametolewa na kampuni ya Rom solution ikiwa ni mwendelezo wa mkataba ulipo kati ya serikali
ya mapinduzi ya zanzibar kupitia wizara ya nchi ofisi ya rais tawala za mikoa idatra malaum za smz katika
kuimarisah ulinzi na usalama.
Zanzibar24.
Comments