Serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi yatoa ahadi katika skuli za mkoa huo.

Serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi imesema itahakikisha inapunguza matatizo yanazozikabili skuli mbalimbali zilizopo katika mkoa huo ikiwepo uhaba wa madawati.

Akizungumza  katika mahafali ya wanafunzi wa kidatu cha sita wa skuli ya sekondari ya Jang’ombe ,katibu tawala wa mkoa wa Mjini Magharibi  Hamida Mussa khamis amesema Serikali inatambua matatizo yanayowakabili wanafunzi na tayari ipo katika hatua ya kuyatatua matatizo hayo.

Amesema Serikali ya Mkoa huo kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo pamoja na watu binafsi imekusudia kuimarisha sekta ya elimu ili kuweza kuzalisha wataalamu watakayoiwezesha serilikali ya Zanzibar kufikia uchumi wa Viwanda.

Katibu tawala huyo pia amechukua fursa hiyo kuwataka wananfunzi kuwa na nidhamu wakiwa madarasani ili kuengeza ufaulu katika mitihani yao wanayotarajiwa kufanya may7 mwaka huu.
Aidha ametowa wito kwa wanafunzi kuendelea kusoma kwa bidii ili kupatia ufumbuzi tatizo la wataalamu wa fani mbalimbali Nchini ikiwemo  wataalamu wa sekta ya Afya na Elimu ambayo ina mahitaji makubwa kwa wananchi.

Kwa upande wake Mwalimu  Mkuu Mstaafu wa Skuli ya Sekondari ya Jang’ombe  Suleiman Mbarouk amesema  ili wanafunzi waweze kufaulu mitihani yao ni vyema kwa walimu kujua wajibu wao katika kuwapatiwa wanafunzi elimu inayoendana na mahitajitaji yao.

Amesema wanafunzi wana mwamko mkubwa wa kusoma masomo yao ila wanarejeshwa nyuma na baadhi ya matatizo wanayokumbana nayo ikiwemo uhaba wa  vifaaa vya skuli na walimu wa kutosha jambo ambalo linarejesha nyuma maendeleo yao.

Aidha ametowa wito kwa wazazi na walezi kuimarisha marikiano kati yao na walimu ili kuwawezesha wanafunzi kufikia malengo waliyoyakusudia katika masomo.

Nae afisa Elimu wa Mkoa wa khatib Tabia ameiomba Bodi ya mikopo ya Elimu ya Juu kuangalia namna ya kuwasaidia wananfunzi wa masomo ya sanaa kupata mikopo ili waweze kujiendeleza kitaaluma.

Amesema wananfunzi wengi wanashindwa kuendelea masomo yao kutoka na kukabiliwa na ugumu wa maisha katika familia zao hivyo watakapo patiwa mikopo itawawezesha  kufikia malengo waliyoyakusudia pamoja na kuengeza wataalamu wa masomo hayo Nchini.
   Awali katika risala ya wanafunzi iliyosomwa na Zulfa Sharif wanafunzi wa skuli hiyo wamesema mbali na kusoma kwa bidii washindwa kufanya vizuri katika masomo yao kutoka na kukabiliwa na matatizo ya uhaba  wa Vitabu,Vifaa vya Maabara na madawati.


Aidha wametowa wito kwa serikali ya Mkoa wa Mjini Mgahribi kupitia kampeni ya MIMI NA WEWE kuwajengea holi litakalotumika kwa shughuli za skuli na shughuli nyenginezo ambazo zinachangia mapato ya kuiendeleza skuli hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugeni wa Sekondari ,Afisa Elimu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Muhammed Aboud amesema Wizara itaendeendelea kuimarisha miundombinu ya skuli zote za Zanzibar ikiwemo upatikanaji wa vifaa vya maabara na Vitabu vya kusomea.
Zanzibar24.

Comments