Seriakali kununua meli nyengine.


SHIRIKA la Meli na Uwakala Zanzibar, lina mpango wa kununua meli nyengine mpya ya abiria na mizigo ili kuondosha changamoto ya usafiri wa abiria, baada ya kukamilika ununuzi wa meli ya mafuta.

Mkurugenzi wa shirika hilo, Ahmada Vuai, alieleza hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, ofisini kwake Malindi.

Alisema lengo la ununuzi wa meli hiyo ni kuondosha changamoto ya usafiri wa abiria kati ya Pemba, Unguja na Dar es Salaam.

Kuhusu meli ya Mv Mapinduzi II, alisema inaendelea na matengenezo na inatarajiwa kuanza safari katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani.

Alisema shirika linaelewa changamoto zinazowakumba abiria lakini waliwaomba kuendelea kuwa wavumilivu katika kipindi  hiki.

Alisema ili kuhakikisha huduma ya usafiri inakuwa endelevu serikali kwa kushirikiana na shirika hilo imekusudia kuifanyia matengenezo makubwa meli ya Mv Maendeleo ili iendelee kutoa huduma ya usafiri wa abiria na mizigo.

Zanzibarleo.

Comments