Mama wajawazito wapata shida Mtambwe Kaskazini, Pemba.


Related imageNa Othman Ali Juma - Pemba
othmanalijuma8@gmail.com
Akina mama wajawazito wanaopatiwa huduma katika kituo cha afya cha uondwe shehia ya mtambwe kaskazini Pemba  wanaendelea kuteseka wakati wanapomaliza kujifungua kutokana na jiko la kupashia maji ya moto(Heater) kuibiwa.

Jiko hilo ambalo lilitumika kwa kupashia  maji ya moto wajawazito pindi wanapomaliza kujifungu ili waweze kujisafisha.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao wanawake hao wamesema ni takribani wiki mbili sasa tokea kuibiwa kwa jiko hilo hivyo wanapohitaji huduma hiyo hulazimika kuhodisha nyumba za jirani zilizopo karibu  na hospitali hiyo hali ambayo inawapa usumbufu mkubwa hususani nyakati za usiku.

Jaria Hamad Bakari ambaye ni mkaazi jirani na hospitali hiyo amesema tokea kuibiwa kwa hita hiyo kumekuwa na usumbufu mkubwa kwa mama wajawazito wanaotoka maeneo ya mbali pindi wanapohitaji maji ya moto.

''Ilipokuwepo hita wazazi walikuwa hawataabiki lakini tokea kuibowa umekuwa ni usumbufu kwa wazazi  na hata  sisi wakaazi wa karibu na hospitali kwani usiku mkubwa kushajipumzisha unakuta   unagongewa  wanataka wasaidiwe maji ya moto'' alisema Jaria.

Mmoja miongoni mwa wahudumu wa kituo hicho Hamida Juma Mohd amesema  uwepo wa heater hiyo ilisaidia kwa kiwango kikubwa kuboresha upatikanaji wa huduma kwa mama wajawazito lakini tokea kuibiwa kwa hita hiyo kumepelekea kudorora kwa utolewaji wa huduma .

Amelezea kuwa kuibiwa kwa jiko hilo kumepelekea kukosa muda mzuri wa kufanya kazi zao kwa ufanisi kwani hulazimika kumuacha mzazi kwa kipindi na kwenda kumtelekea maji hali ambayo ni usumbufu kwao na kwa wagonjwa pia.

Aidha amesema kuwa ili kupunguza usumbufu wanaoupata huwashauri mama wajawazito wanakuja kituoni hapo  kujifungua kuchukua maji yao katika chupa.

Nae  msimamizi wa kituo hicho Zainab Hassan Sheha amesema mnamo majira ya saa kumi na mbili asubuhi alipokea taarifa hizo kwa njia ya simu kutoka kwa mfanyakazi mwenzake  na wakati huo huo kuchukuwa uwamuzi wa kumpatia tarifa hizo DMO pamoja na sheha na kumelekeza kuweka ripoti kituo cha polisi.

Sheha amesema kuwa kutokana na kutokuwepo kwa mlinzi katika kituo chao kunachangia kwa kiasi kikubwa kufanyika kwa hujuma hizo hivyo ameiyomba serikali kupitia wazara ya afya kuwawekea mlizi hospitalini hapo.

Kwa upande wake  sheha wa shehia hiyo Suleiman Bakar Khamis amesema amelipokea tukio hilo  kwa masikitiko makubwa na kutoa wito kwa jamii yeyote aliyechukua jiko hilo kulirejesha mara moja na kusema kuwa kuibiwa kwa hita hiyo si hasara kwa kwake tu bali ni kwanajamii wote wa Mtambwe.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi wa mkoa wa kaskazini Pemba Haji Khamis Haji amesema mnamo tarehe 26 majira ya asubuhi waliripotewa tukio hilo na hadi sasa  wanaendelea na uchunguzi kubaini ni nani aliyehusika na tukio hilo.

Kamanda haji ametoa wito kwa wanajamii wa Mtambwe  kushirikiana na jeshi la polisi kwa kulipatia taarifa ili kuhakikisha wanafanikiwa kumkamata aliyetenda kosa hilo.

Comments