Hofu ya kusimama kwa huduma za kijamii yatanda kwa wananchi wa Mtambwe Pemba.


Na Othman Ali Juma - Pemba
othmanalijuma8@gmail.com

Wananchi wa shehia ya mtambwe kaskazini Pemba wanahofu ya kusimama kwa huduma za usafiri na  shughuli zao za kiuchumi  kutokana na kalafati ya barabara yao kughariki hali inayowapa wasi wasi kuwa  muda wowote kutoka sasa njia hiyo inaweza kukatika.

 Wakizungumza  huko kijijini kwao wananchi hao wamesema iwapo kama serikali haitofanya juhudi za haraka kuzibiti daraja hiyo isiendelee kughariki muda wowote kutoka sasa njia hiyo itakatika na kupelekea kusimama kwa huduma zao muhimu za kimaisha.

Bakari Mwita Sheha na Omar Fakih Hassan wakaazi wa kijiji cha uondwe  wamesema  kuwa asilimia 75 shughuli za kiuchumi za wanamtabwe  zinategemea uwepo wa barabara hiyo hivyo iwapo kama haitofanyiwa matengenezo ya haraka itapelekea athari kubwa kwa wanamtabwe.

 ''Kama daraja ya mpaka njia itaachiwa ikatike basi kijiji cha uondwe na kele ambako ndio kwenye  standi za gari za mtambwe watakosa huduma ya usafiri,pia itakuwa ni dhiki sana kwa wanachi kusafirisha bidhaa zao kama vile ndizi,Muhogo   na nyenginezo kupeleka mjini ili kutafuta soko''.walisema wanakijiji hao.

Wamesema kuwa licha ya kusimama kwa shughuli za kiuchumi lakini pia kutapelekea kutokupatikana kwa huduma muhimu za afya pindi wanapolazimika kuzifuata maeneo mengine ambayo ni  nje ya Mtambwe.

''Inapotokea mtu kaumwa na maradhi makubwa ambayo hayawezekani kutibiwa hapa hutupasa kumpeleka Wete au Chake Chake jee njia ikiachiwa ikatike tutamuduje kumpeleka huko''.walisema.

Akisibitisha kughariki kwa daraja hiyo ya Mpaka njia Sheha wa shehia ya Mtabwe Kaskazini Suleiman Bakar Khamis amesema kwa takribani wiki moja sasa tokea kughariki kwa kalafati hiyo na  baada ya kuona hali inaendelea ndipo alipoamua kupiga simu kunako husika na baada ya kuona hakuna hatua waliyoichukua akamua kumpigia simu waziri.

''Baada ya kuona hali hii nilitoa taarifa akaja Dr. Sira,Mh,Said Soud na Mh,Juma Ali Khatib wakaiyona hali ya njia ilivyo ila nilipoona siku zinakwenda hakuna hatua waliyoichukua na hali ya njia inazidi kuwa ngumu niliamua kumpigia Mh, waziri Dr, Sira Ubwa Mamboya.amesema sheha huyo.

Aidha amesema  ni jambo la aibu kuwa njia tokea ifunguliwe na Mh, Rais hata miaka mitatu haijafika  sasa inaaza kukatika  hivyo ametoa wito kwa mainjiania wa ndani kuwa makini pindi wanapowakabidhi  kazi makampuni kutoka nje kuhakikisha wanajenga kwa viwango vinavyotakiwa ili kuepu kupoteza mamilioni ya pesa ambazo zinahitajika kwa kuboresha huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake Afisa Mdhamini Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano  na Usafirishaji Hamad Ahmed Baucha amesema kwa sasa wanaendelea na ujenzi wa kalafati hiyo na baada ya siku tatu inatarajiwa kukamilika .

Baucha  amewataka wanamtambwe kuwa wavumilivu kwa kipindi hichi na kuwataka kutoa msaada wao pindi unapohitajika ili kukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa.

Baraba ya Mtambwe ilikamilika ujenzi wake na kufunguliwa na Mh, Rais wa Zanzibar Dr, Ali Mohd Shein si zaidi ya miaka Mitatu iliyopita ambapo kwa sasa kutokana mvua zinazoendelea kunyesha imeghariki katika daraja la Mpaka njia na kukatika katika eneo la Kisalani.


Comments