Siku
ya May 1 , msanii wa bongo movie Aunty Ezekiel alikuwa na press
conference kwa ajili ya kuitangaza filamu yake mpya inayoitwa mama
ambayo amemshirikisha mtoto wake wa kike Cookie.
Akiongea
na waandishi wa habari, mama cookie anasema kuwa hakuamua kumshiriksha
mume wake moze iyobo kwa sababu anaamini kabisa kila mtu amezaliwa na
kipaji chake hivyo anajua kuwa kuigza sio kazi ya Moze.
Aunty
anasema kuwa aligundua kuwa mtoto wake ana kipaji lakini yeye kuwa na
mahusiano na moze haimaanishai kuwa basi amlazimishe Moze kufanya movie
wakati anajua kuwa moze hawezi kuigiza bali anaweza kucheza na ndio
ilivyo hata kwake kuwa hawezi kucheza kwahiyo, kuna baadhi ya vitu kati
ya ke na moze vitabai kuwa kama vilivyo.
"Mimi
na Moze tuna mipaka, tumekuwa tukiihsi bila kuingiliana katika
kazi,mimi siingiliani nae katika kazi zake, na yeye pia haingilii kwenye
za kwangu hapana.
"Kwahiyo
nisingependa kulazimisha kwa sababu eti ni mama aliyezaa nae, kwaio
sijamshirikisha kwa sababu kipaji chake ni cha kucheza na sio kuigiza.
Moze
kwangu ana mchango mkubwa sana , mchango wake ni mkubwa sana zaidi hata
ya pesa kwa sababu ninapokuwa nikipata ushauri wake na nikaufanyia
kazi ndio unaokuwa unaniletea pesa."
Comments