
Ili kufikia malengo hayo ni lazima pawepo na ushirikianao mkubwa kwa
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, pamoja na taasisi na watu wengine,
jambo ambalo litaleta faida kubwa kwa vijana hao.
Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Omar Hassan
Omar ‘King’ alitoa kauli hiyo katika ukumbi wa skuli ya Haile Salasi
wakati akifungua mashindano ya Sanaa ya Maigizo na Uchoraji, kwa mkoa wa
Mjini Magharibi yaliyoshirikisha skuli tisa za mkoa huo.
Alisema kuwa kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuendeleza
utamaduni ambapo mikakati maalum imepangwa kulifanikisha jambo hilo, kwa
kulifanya jambo hilo kuwa endelevu.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa, Sensa, Filamu na
Utamaduni Dk. Omar Abdalla Adam, alisema kuwa mashindano hayo
yatafanyika kwa mikoa yote ya Zanzibar, ambapo wameanza na Mkoa wa Mjini
Magharibi.
Alisema kuwa mashindano hayo yatafanyika kwa miaezi mitatu na
watashirikisha fani ya sanaa ya maigizo na uchoraji, kwa mikoa ya
Zanzibar na baadaye kutafuta bingwa wa taifa.
Chanzo: Zanzibarleo
Comments