
Akizungumza katika Uzinduzi wa kituo cha
utotoaji wa watoto wa samaki Hatchery huko Beit Ras amesema serikali
imekuwa ikichukua juhudi mbalimbali katika kukuza na kuimarisha sekta
ya uvuvi kwa kutafuta wadau wa maendelo kuekeza katika sekta huu
muhimu ambazo zinachangia katika kukuza na kuongeza kasi ya ukuwaji wa
uchumi Zanzibar ikiwemo uvuvi,ufugaji,kilimo na utalii.
Amesema uzinduzi wa kituo hicho cha
kuzalishaji wa watoto wa samaki kitasaidia katika kuwaondolea
usumbufu unaowapata wafugaji katika upatikanaji wa watoto hao kwani
itaongeza uzalishaji na kusema wakati umefika kwa wafugaji kubadilika
na kuachana na ufugaji wa mazoea ambao hauleti tija kwao na taifa na
badala yake sasa kufuga kwa ajili ya biashara na chakula ili kuweze
kupata soko ndani na nje ya nchi.
Aidha Balozi Seif amesema endepo wavuvi
na wafugaji watautumia vyema mradi huo utaweza kusaidia katika
upatikanaji wa samaki wengi Zanzibar ambao watachangia katika kukuza
na kuongeza upatikanaji wa chakula kiurahisi pamoja na kuongeza
pato la taifa ambapo awali sekta ya uvuvi inaongeza asilimia 10
katika pato la taifa.
Amesema lengo kuu la kuanzishwa mradio huo
katika kituo hicho cha kutotolea samaki ni kurahisisha upatikanaji
wa vifaranga vya samaki kwa wananchi ambao ni
wafugaji lakini pia ni kuondoa tatizo la ajira kwa vijana kwani
kituo hicho kitakuwa na fursa za upatikanaji wa ajira pamoja na
kupanua wigo katika sekta ya uvuvi kuweza kuleta maendeleo endelevu.
Hata hivyo Makamu wa Rais wa Zanzibar
amesema mashirika ya maendeleo yakiwemo FAO na Korea International
Agency KOICA yamekuwa yanatoa michango mikubwa katika kukuza na
kuendeleza Zanzibar katika sekta mbalimbali ambazo
zinachangia kuondoa umaskini na kuleta na kuleta maendeleo ili kufikia
uchumi wa kati hivyo wananchi hawana budi kuunga mkono juhudi na
harakati zinazokuchukuwa na serikali pamoja na mashirika hayo ili
Zanzibar iweze kuendelea.
Kwaupande wake Rais wa KOICA Mikyung Lee
amesema Wataendeleo kuiunga mkono Zanzibar katika kuharakisha maendeleo
ya nchi hiyo ambapo amesema mbali na kusaidia katika sekta ya uvuvi
na kilimo lakini pia wataendelea kuisaidia Zanzibar katika sekta ya
elimu ili kukuza vipaji kwa vijana ambapo wametenga zaidi ya Dolla
Million 15 za marekani ili kutumika katika sekta hiyo.
Lee amesema pia nchi ya korea haita kuwa
nyuma katika kuongeza juhudi kwenye sekta ya afya kusaidia kutokomeza
ugonjwa wa kipindupindu unaowasumbua wananchi na serikali kila ikifika
kipindi cha mvua za masika ambapo amesema yote hayo ni kuiunga mkono
serikali ya Zanzibar ili kuleta maendeleo nchini na kuweza kufikia
uchumi wakati.
Amesema Zanzibar inanafasi kubwa katika
kukuza uchumi wake kutokana na kuwa na rasilimali nyingi zenye kuuzika
ndani na nje ya nchi ikiwemo rasilimali za baharini zinazovutia
katika kuongeza pato la taifa hivyo wananchi wazidi kuhamasika katika
kutumia rasilimali hizo muhimu ili kupunguza umaskini.
Nae Katibu Mkuu Wizara ya
Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Zanzibar Maryam Abdalla Mabodi amesema
Vikundi mia moja na arobaini na nne zipo Zanzibar unguja na pemba
zinavyofuga samaki hivyo uwepo wa kituo cha kutotolea watoto wa samaki
kitawasaidia pamoja na mabwawa matano yameanzishwa ili kuongeza kasi ya
uzalishaji wa samaki.
Katibu Mkuu huyo amewataka wananchi
wanaoishi karibu na bahari kutumia fursa za uwepo
wa bahari katika kuzalisha samaki wakiwemo kaa,kamba,chaza na
majongoo ya pwani ili kuweza kujipatia kipato pamoja na kukuza sekta
ya ufugaji na utalii.
Amesema lengo la uzalishaji huo wa watoto
wa samaki ni kuzalisha zaidi ya watoto Elfu 10 kila mwaka ambapo jumla
ya Dolla Million tatu laki mbili na Ishirini na nane elfu za Marekani
zimetumika katika kuwezesha mradi huo wa kutotoa watoto wa samaki
Zanzibar ambao ni mradi wa kwanza kwa ukubwa kwa Afrika.
Zanzibar24ز
Comments