
“Nilikuwapo mahakamani leo kuonyesha mshikamano kwa
Viongozi wenzangu waliofikishwa mahakamani kwa kinachoitwa uchochezi.
Nawaambia Watanzania Mfumo wa Demokrasia ya Vyama vingi nchini upo
hatarini kubomolewa,” Zitto aliandika facebook.
Aliongeza, “Tangu tuanze siasa za vyama vingi nchini
sijapata kuona tishio kubwa kama hili la kuwasweka ndani Viongozi
theluthi 2 ya Viongozi wa Kitaifa wa Chama kikubwa Cha pili cha Siasa
nchini. Jambo la kushangaza zaidi ni ukimya usio kifani wa wanachama wa
Vyama vya Siasa vya upinzani nchini. Tukiendelea hivi, amini nawaambia,
Demokrasia ya vyama vingi inafutwa,”
Chadema kimelaani vikali kukamatwa kwa viongozi wao:
“Zimekua ni sarakasi dhidi ya upinzani. njama hizi dhidi viongozi wetu
hatutaweza kuzinyamazia, tutaendelea kuzilaani na tunaangalia uwezekano
wa kuchukua hatua za kisheria” Afisa habari wa Chadema Tumaini Makene ameileza BBC.
Bwana Makene amesema viongozi wa Chadema ambao wamekuwa wakiripoti
polisi kwa tarehe zilizokuwa zimepangwa, ilikuwa ni siku yao ya kufika
kituo cha Polisi.
chanzo: zanzibar24.
Comments