
Akizungumza na Zanzibar24 amesema hivi
sasa wanawake wamekuwa na muamko wa kutosha katika kujishughulisha na
harakati za maendeleo, ambapo amesema hatua hiyo imetokana na elimu
inayotolewa na chama cha waandishi wa habari wanawake Zanzibar tamwa
pamoja na taasisi nyengine nchni zinazoshughulikia masuala ya wanawake.
Hata hivyo Dr Mzuri amesema licha ya
elimu wanazopewa wanawake katika kujishughulisha katika harakati za
maendeleo lakini tatizo kubwa linalowakabili wanawake wengi hivi sasa ni
elimu ndogo na wengine hawajasoma kabisa hali inayowakwamisha katika
kutangaza bidhaa zao.
Kwaupande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya
wafanyabiashara wa viwanda Dr.Mohammed Hafidhi
amewataka wajasiriamali wanaozalisha bidhaa nchni kuongeza thamani ya
bidha zao kwa kuzifanyia ubunifu utakaowavutia wateja kuweza
kuzinunua ili wahakikishe wanazingatia suala la usafi wakati
wanapotengeneza bidhaa hizo ili kulinda afya za walaji.
chanzo: Zanzibar24.
Comments