
Mbowe na wenzake wameshafikishwa mahakamani hapo wakitokea mahabusu
ya Segerea wakikabiliwa na mashtaka nane yakiwemo kufanya maandamano
yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT),
Akwilina Akwiline, Februari 16, mwaka huu, uasi na kuhamasisha chuki.
Wengine waliofikishwa mahakamani ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji
Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho (Zanzibar) Salum
Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Bara) na Mbunge wa Kibamba,
John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chama hicho Vicent Mashinji na wengine.
Baadhi ya wabunge wa Chadema, wafuasi wa chama hicho na wananchi
wengine waliofika mahakamani kufuatilia kesi hiyo ni Waziri Mkuu
Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, Waziri Mkuu
Mstaafu, Fredrick Sumaye, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Prof.
Abdallah Safari, Mbunge Joseph Haule ‘Prof. Jay.
Comments