KLABU za Real Madrid na Liverpool zimefuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kufuatia matokeo yao mazuri ya mechi za marudiano zilizochezwa juzi.
Ikiwa ugenini nchini Ufaransa,Real Madrid iliwalaza wenyeji PSG
magoli 2-1 huku Liverpool ikilazimishwa sare 0-0 katika uwanja wa
Anfield.
Cristiano Ronaldo alifunga bao lake la 12 kwenye michuano hiyo kabla
ya Casemiro kuongeza la pili huku lile la kufutia machozi la PSG
likifungwa na Edinson Cavanni.
Sare ya bila ya kufungana nayo iliwapeleka Liverpool robo fainali
huku golikipa wa FC Porto Iker Casillas akiweka rekodi katika mchezo huo
kwa kuwa kipa wa kwanza kucheza na Liverpool katika ligi hiyo msimu huu
bila ya wavu wake kuguswa.(AFP)
Comments