
Akizungumza katika Shamrashamra za maadhimisho ya kuelekea katika siku ya wanawake duniani huko Ngomekongwe amesema serikali inatambua kuwa wanawake wajasiriamali wanakabili na matatizo mbalimbali licha ya kuwa na muamko wa kujiunga na vikundi mbalimbali vya kujiendeleza kiuchumi ambapo amewataka kutovunjika moyo kwani sera zilizopo zitaweza kuwanyanyua wanawake katika kufikia dira ya maendeleo nchini.
Amesema mashirikiano baina ya wajasiriamai , serikali pamoja na wadau wa maendeleo ni jambo litakalo saidia kufikia uchumi wa kati na kuweza kukuza gurudumu la maendeleo lakini pia kujitengemea wenyewe bila ya kuwa utegemezi kutoka serikalini.
Aidha Balozi Amina amezitaka taasisi mbalimbali zinazosimamia masuala ya wanawake kuhakikisha kuwa mifumo yote iliyopo ya maendeleo inakuwa rafiki na inalenga katika kuyaendeleza makundi yote ili kufaidika na mipango ya maendeleo kama ilivyodhamira ya serikali ya kufikia uchumi wa kati wa viwanda.
Amesema Ujio wa viwanda vidogovidogo na kati Zanzibar vitawasaidia wananchi wengi hasa wafanyabiashara za wajasiriamali kuuza bidhaa zao kwa urahisi na hatua hiyo inawawezesha kuzalisha bidhaa zao kwa wingi na vyenye ubora.
Mapema Mkurugenzi Jumuiya ya waandishi wa habari wanawake Zanzibar tamwa Dr Mzuri issa amesema lazima serikali iwaunge mkono wanawake ili kuondoka katika mifumo dume ya utegemezi kwani hali hiyo itawasaidia kutodhalilishwa na waume zao pamoja na wao kukomboka katika hali gumu ya maisha.
Hata hivyo Mzuri amesema elimu bado inahitajika kwa wananchi juu ya kuona umuhimu wa kutumia bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali wa ndani kwani hatua hiyo inasaidia kukuza soko la ndani ya nchi.
Amesema tayari wanawake wengi hivi sasa wameelimika katika masuala ya ujasiriamali pamoja na kuwa na muamko wa kumiliki ardhi lakini wanarudishwa nyuma na baadhi ya taasisi kutowapa mashirikiano mazuri pindi wanapohitaji huduma au msaada kutoka kwao hivyo serikali ihakikishe inasimamia watendaji wake ili kuona changamoto hizo zinaondoka kwani ndio miongoni mwa vikwazo vinavyopelekea wanawake kushindwa kufikia malengo yao.
Kwaupande wake Msoma Risala katika Maadhimisho hayo kwa niaba ya wanawake wa Zanzibar Jina Pandu amesema kukosekena kwa malighafi za uhakika za kuzalisha bidhaa zao itapelekea wao kushindwa kuzalisha vizuri bidhaa zenye ubora hivyo serikali ihakikishe inawasaidia wajasiriamali ili kuweza kupata malighafi kwa urahisi.
Hata hivyo amesema kukosekana kwa mashirikiano kwa baadhi ya taasisi za serikali kunachangia kuduma uzalishaji wa bidhaa zao hasa taasisi zinazotoa huduma za maji safi na salama zawa pamoja na taasisi zinazotoa huduma za umeme zeco zinawarudisha nyuma kwani wakikosa huduma hizo hushindwa kufanya shughuli zao.
Wakati huo huo wametoa wito kwa serikali kuziomba mamlaka zinazohusika na kukusanya mapato kuwapunguzia kodi wajasiriamali wadogo kwani wanashindwa kumudu gharama za kodi kutokana mitaji yao ni midogo ukilingamishwa kodi wanazotozwa.
Maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani yanatarajiwa kuadhimishwa tarehe 8 ya mwezi Murch mwaka huu ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni Tubadilishe mifumo iliyopo na sera ili wanawake wote wafaidike na maendeleo ya kiuchumi,kijamii na kisiasa.
chanzo:Zanzibar24.
Comments