
Wakizungumza baadhi ya
Vijana wanaojishughulisha na fani ya uchongaji wamesema licha ya
kuitumia fursa ya kujiajiri wenyewe ili kuondokana na tatizo la
ajira lakini bado katika fani hiyo wanakabiliwa na tatizo la
upatikanaji wa mbao kwa ajili ya kutengezea vifaa vya matumizi ya
nyumbani na maofisini.
Wamesema hivi sasa vijana wengi wamekuwa
na muamko wa kujifundisha fani mbalimbali ili kuweza kujiajiri lakini
wanakabilia na tatizo la mitaji na vifaa vyenye ubora kufanikisha kazi
zao ili kuweza kuwaingizia kipato.
Wamesema mbali na yote lakini tatizo la
kuadimika kwa miti inayotumika kwa ajili ya mbao inawapa ugumu katika
kazi zao za uchongaji hivyo serikali imeombwa kuwasaidia wananchi hasa
vijana walijishughulisha katika fani hiyo kuweza kuwapunguzia ushuru
pindi wanapokwenda kununua mbao nje ya Zanzibar.
Aidha mafundi hao wamewataka vijana
kutovunjika moyo katika kufanya kazi licha ya kuwa bado kuna changamoto
nyingi zinazopelekea kuwakwamisha lakini wavumilie ili kuweza kupata
riski za halali.
chanzo: Zanzibar24.
Comments