Mchezo huo uliopigwa huku kijua kikali kikiwaka uwanjani hapo, timu
hizo zimeshuka uwanjani Wawi ikiwa na pointi 22 ikishika nafasi ya 10,
huku Chuo Basra ikiwa na pointi 17 ikishika nafasi ya 13 katika ligi
hiyo.
Timu hizo zilikianza kipindi cha kwanza kwa kasi kubwa huku kila timu
ikihitaji ushindi uwanjani hapo, kila timu ikikosa mabao ya wazi baada
ya washambuliaji wa timu hizo kutokuwa makini.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kubwa, kila timu ikifanya
mabadiliko ya wachezaji wao, ili kuweza kupata bao la kuongoza ,
mabadiliko hayo yaliweza kuwasaidia Wawi Star dakika ya 59 kwa kuandika
bao lililofungwa na Sadam Maulidi.
Comments