Balozi wa Marekani nchini Mauritania azomewa na wanafunzi na kulazimika kukimbia sherehe.

Balozi wa Marekani nchini Mauritania azomewa na wanafunzi na kulazimika kukimbia shereheKelele za malalamiko za wanafunzi nchini Mauritania juu ya maamuzi ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuutambua mji wa Quds (Jerusalem) kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel, zilimlazimu balozi wa Marekani nchini humo, kukimbia sherehe zilizofanyika mjini Nouakchott.

Awali Michael Dodman, balozi wa Marekani nchini Mauritania alikuwa amehudhuria sherehe katika kituo kidogo cha mafunzo ya lugha ya Kingereza katika Taasisi ya Elimu ya Juu ya Utalii na Utafiti ya Kiislamu mjini Nouakchott. 
Hata hivyo kelele za malalamiko zilizofanywa na wanafunzi waliokuwa wakilaani hatua ya Rais Trump ya kuutaja mji wa Quds kuwa mji mkuu wa utawala bandia wa Kizayuni, zilimfanya Dodman, kuondoka katika sherehe hizo haraka.
Kadhalika kelele hizo za wanafunzi zililaani uamuzi wa serikali ya Marekani wa kutaka kuhamisha ubalozi wa nchi hiyo kutoka Tel Aviv na kuupeleka Baitul-Muqaddas.
Itakumbukkwa kuwa, tarehe sita Disemba mwaka jana, Rais Donald Trump wa Marekani na licha ya kuwepo upinzani mkubwa kieneo na kimataifa, aliutangaza mji huo wa Quds kuwa ni mji mkuu wa utawala haramu wa Israel, suala ambalo lilikabiliwa na radiamali kali kutoka duniani.
chanzo:parstoday.

Comments