
Akizungumza na Zanzibar24 Afisa Habari wa Mamlaka hiyo Mwanaidi Suleiman amesema zaeca kupitia kitengo hicho ilifanya msako maalumu na kufanikiwa kuwakamata watu hao katika eneo la kianga, kwarara na kilimani Mjini unguja ambapo kesi hiyo tayari imesha kamilika uchunguzi wake na hatua inayofata sasa ni kuwafikisha katika ofisi ya DDP ili kupelekwa mahakamani.
Akiwataja watu hao ni Faustian Amiri Salum mwenye umri wa miaka 42 amekamatwa na mafurushi 40 ya bangi ,Ismail Haji Habibu mwenye umri wa miaka 20 amekutwa na kete 250 za unga aina ya heroin na Mussa Shabani ambae amekutwa na kete 19 za madawa ya kulevya aina ya heroin.
Aidha Mwanaidi amewataka wananchi kuzidisha mashirikiano katika kuwafichua wasambazaji wa madawa ya kulevya nchini ili kupunguza ongezeko la watumiaji wa dawa hizo.
chanzo:Zanzibar24.
Comments