Shirika la habari la Mehr limemnukuu Dk
Ali Akbar Velayati akisema hayo jana usiku katika mkutano wa wanafunzi
wa vyuo vikuu wanaounga mkono Intifadha ya Palestina huko Mash'had,
kaskazini mashariki mwa Iran na kuongeza kuwa:
Kwa miaka kadhaa sasa
Marekani imekuwa ikifanya njama za kuzisambaratisha nchi za eneo hili na
kuunda Mashariki ya Kati Kubwa lakini imeshindwa. Amesema, matukio ya
Libya, Syria, Iraq na Yemen ni sehemu ya njama hizo za Marekani.
Velayati amelaani vikali njama hizo za
Marekani zenye shabaha ya kuzisambaratisha nchi za eneo hili na kusema
kuwa, hata harakati mpya za hivi sasa za kijeshi za Marekani nchini
Syria zinafanyika kwa lengo hilo hilo la kuzigawa nchi za Mashariki ya
Kati.
Amesema, Wamarekani kamwe hawatafanikiwa
katika uadui wao wa kuigawa vipande vipande Syria na kwamba imma
watatoka wenyewe mashariki mwa Mto Furati au taifa la Syria litawatimua
katika eneo hilo.
Vile vile amesema, Hizbullah ya Lebanon
imekuwa imara sana kwa msaada wa Iran kiasi kwamba hivi sasa majenerali
wa kijeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wanakimbia kuingia vitani na
Hizbullah. Amesema, hata katika vita vya Ghaza pia, Wazayuni wamekwama
kutokana na muqawama wa wananchi mashujaa wa Palestina.
chanzo: parstoday.
Comments