UN: Magendo ya binadamu inaongezeka Libya.

UN: Magendo ya binadamu inaongezeka LibyaWataalamu wa Umoja wa Mataifa wametahadharisha kuhusu ongezeko la magendo ya binadamu nchini Libya.

Waraka wa siri uliokabidhiwa kwa wanachama 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa unasema kuwa, tangu wanachama wa kundi la kigaidi la Daesh walipofukuzwa katika eneo la Sirte mwaka 2016, wamekuwa wakifanya jitihada za kuwa karibu zaidi na wafanya magendo ya binadamu nchini Libya. 
Ripoti hiyo ya siri yenye kurasa 157 inasema kuwa, magendo ya binadamu na ukiukaji wa haki za binadamu unaongezeka sana nchini Libya.
Wataalamu wa Umoja wa Mataifa waliotayarisha ripoti hiyo pia wanasema, kuna wasiwasi kwamba makundi ya waasi na wafanya magendo ya binadamu yanatumia suhula za dola kwa ajili ya kudhamini njia za kusafirishia wahajiri haramu. 
Wamesema kuwa kundi la Daesh ambalo kimsingi linaundwa na wapiganaji wa kigeni limetuma wawakilishi kadhaa wakiwa na pesa talimu huko kusini mwa Libya kwa ajili ya kuwasiliana na wafanya magendo ya binadamu. 
Wafanya magendo ya binadamu wamekuwa wakitumia hali ya ukosefu wa amani nchini Libya kwa ajili ya kusafirisha binadamu na kuwauza barani Ulaya na maeneo mengine ya dunia.     
chanzo:parstoday.

Comments