SMZ: Ofisi ya muft haina malaka ya kusikiliza kesi za migogoro za usimamizi wa mali za taasisi za dini.


Akijibu swali katika kikao cha Baraza la Wawakilishi Chukwani, Naibu Waziri wa Nchi OR Katiba na sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Khamis Juma Mwalimu amesema Ofisi ya Mufti itaendelea na majukumu yake ya kutoa suluhu ya kesi na sikukutoa hukumu za Migogoro ya Usimamizi wa Mali za dini.
Amesema licha ya Ofisi hiyo kutoa suluhu lakini Baadhi ya Wananchi wanakimbilia Mahakamani kutokana na kutoridhika kwa suluhu hiyo ili waweze kunufaika na haki zao za msingi.
Amesema kwa kipindi cha Mwaka 2015 hadi Disemba 2017 jumala ya kesi 29 za usimamizi wa mali za Miskiti ambapo kwa upande wa kesi za mirathi ni 260 zimefunguliwa katika mahkama kuu.
chanzo:Zanzibar24.
Comments