
Akizungumza na Zanzibar24 amesema ni vyema
Watu wenye ulemavu kupewa haki sawa za kimaendeleo na watu wengine
wasokuwa na ulemavu ili kila mmoja wao ajihisi huru kama wengine kwani
nao wakiwezeshwa wanaweza.
Aidha Mkurugenzi Asya amebainisha kuwa
bado watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto nyingi katika
jamiii ikiwemo ukosefu wa vifaa wanavyotumia kwa shughuli zao za kila
siku kama vigari vya kutembelea, Fimbo, Miwani na kadhalika.
Hivyo muda imewadia kwa taasisi za
maendeleo na serikali kusimama kidete kuwaondolea usumbufu Wenye
Ulemavu na Wasiojiweza nchini.
chanzo: Zanzibar24.
Comments