Rais wa FIFA awasili nchini leo.

Hatimaye rais wa Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA, Gianni Infantino amewasili nchini majira ya saa 10 : 30 alfajiri ya kuamkia leo na kupokelewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK Nyerere
Infantino atakuwa hapa nchini kwaajili ya mkutano mkuu wa mwaka wa FIFA unaotarajiwa kuanza leo Februari 22 katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere huku ukitegemewa kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wa Shirikisho hilo.

Baada ya kuwa hapa nchini, Infantino ataonana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli.

Mkutano huu wa viongozi wa FIFA na CAF umebeba ajenda mbalimbali  ikiwemo kujadili Maendeleo ya Soka la Wanawake, Maendeleo ya Soka la Vijana, Utaratibu wa kusaidia Vilabu vya soka pamoja na vipaumbele mbalimbali vya kukuza soka kwa nchi za Afrika.

Rais wa FIFA alimhakikishia Waziri Mwakyembe ushirikiano katika masuala mbalimbali ya mpira wa miguu.  Aidha, Rais wa Fifa alisema chaguo la kufanyia mkutano huo Tanzania limetokana na maendeleo ya kasi ya tasnia ya mpira wa miguu na weledi wa viongozi wa TFF waliopo madarakani.

Aidha Rais wa FIFA, Gianni Infantino amemuambia Waziri Mwakyembe kuwa FIFA ni Shirikisho lililo la kweli na lenye uwazi na ndiyo maana wapo Tanzania kwakuwa ni sehemu ya ulimwengu ambao soka linachezwa nakuja nchi hii kuna mchezaji bora wa Afrika anaechezea KRC Genk akitokea hapa ambaye ni Mbwana Samatta.

Infantino anatarajiwa kuondoka nchini mara baada ya kumaliza mkutano wake na kushiriki chakula cha jioni.
chanzo: zanzibar24.

Comments