Shirika la Habari la Palestina limearifu kuwa, Hanna Issa mkuu wa Baraza la Kiislamu-Kikristo la Kuunga Mkono Quds amesema uamuzi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuwatimua Wakristo kutoka mji wa Quds na kutoza kodi majengo ya Wakristo ni matokeo ya uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuutambua mji huo kama mji mkuu wa utawala bandia wa Israel.
Hannan Issa ameongeza kuwa, uamuzi wa Marekani dhidi ya Quds kimsingi ulikuwa ni idhini kwa utawala wa Kizayuni wa Israel uimarishe satwa yake ya kibeberu katika Quds Tukufu na ni kwa sababu hii ndio utawala huo ghasibu sasa unatekeleza kampeni maalumu ya kuwatimua watu wasio Mayahudi kutoka katika mji huo.
Mkuu wa Baraza la Kiislamu-Kikristo la Kuunga Mkono Quds amesema utawala wa Kizayuni unatoza nyumba za Wakristo kodi mjini Quds kwa lengo la kutumia fedha hizo kuchangia katika ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na pia kuwawekea Wakristo vigingiti zaidi.
Gazeti la Kizayuni la Israel Hayom limeandika hivi karibuni kuwa, Baraza la Mji wa Quds ambalo linafungamana na utawala wa Kizayuni wa Israel linalenga kukusanya kodi kutoka katika majengo 887 yanayomilikiwa na kanisa na Umoja wa Mataifa mjini humo ambapo pato hilo la kodi linakadiriwa kuwa karibu milioni 200 kwa mwaka.
chanzo:parstoday
Comments