Kwa mujibu wa wizara hiyo, askari wa
Algeria wamefanikiwa kuangamiza magaidi wawili akiwemo Hisham Abu
Rawaha, mkuu wa propaganda wa mtandao wa al Qaida kaskazini mwa Afrika,
katika operesheni iliyofanywa na askari hao kwenye eneo lililoko umbali
wa kilomita 400 mashariki mwa mji mkuu, Algiers. Magaidi hao hatari
walikuwa wanasakwa na askari wa Algeria tangu mwaka 1994.
Magaidi wengine wawili wameangamizwa na
jeshi la Algeria katika wilaya ya al Madiyah lililloko umbali wa
kilomita 80 kusini mwa mji mkuu Algiers.
Siku ya Ijumaa pia wizara hiyo ya ulinzi
ya Algeria ilitangaza habari ya kuangamizwa magaidi wanane hatari
wakiwemo viongozi kadhaa wa mtandao wa al Qaida katika mkoa wa Khinlash.
Nchi nyingi zinazopakana na Algeria kama
vile Libya, Mali na Niger hazina hali nzuri ya kiusalama hasa kutokana
na kuripotiwa hivi karibuni kwamba baadhi ya makundi ya kigaidi
yameligeuza eneo la kaskazini mwa Afrika kuwa kambi yao kuu baada ya
kushindwa katika nchi kama za Iraq na Syria.
chanzo: parstoday.
Comments