Matembezi na ukaguzi waanza katika kuadhimisha miaka 41 ya CCM.

File:Chama Cha Mapinduzi Logo.png

Viongozi na wanachama wa Chama cha  Mapinduzi Wilaya ya Mkoa wa Mjini Unguja wamefanya matembezi ya kukaguwa wagonjwa hospital  ya mnazi mmoja wodi za watoto [dodoma]  ikiwa ni shamra shamra za maazimisho ya kutimiza miaka  41 ya kuzaliwa kwa chama hicho 
.

Mwenyekiti wa Mkoa  wa Mjini Magharibi Talibu Ali Talib ambae ni mgeni rasmi katika ziara hiyo amesema  kuwa watazidi kutoa misaada kadri ya uwezo wao  na kusaidia wenye matatizo na wasojiweza.


Kwa upande wake Mgurugenzi Utawala, Utumishi Idara ya Mnazi mmoja Hospital  amesemalicha ya changamoto walizonazo pia wapo tayari  kupokea misaada wakati wowote kutoka kwa mashirika mbali mbali.


Dr bingwa wa watoto  Amour Ali Amour amesema kuwa amefrahishwa na ujio wa viongoz hao pia amewaushauri wawe na moyo wa kuendeleza kusaidia na watafurahi zaidi wakiwasaidia chombo ambacho kitaweza kuwasaidia watoto kufyonza umanjano [photosarap mashine].


Rahma Makame Hussen kwa niaba ya wazazi wenzake wenye wagonjwa spital wamesema wameshukuru sana kwa msaada walioupata na kuwataka watu wenye uwezo kusaidia dawa mahospital na kuwasaidia wasojiweza ‘’’

Comments