Makamu Mwenyekiti wa Ada Tadea atoa wazo kwa Wanasiasa.

Makamu Mwenyekiti wa  chama cha Ada tadea  Zanzibar Juma Ali Khatibu amewataka  viongozi wa kisiasa  nchini  kuacha tabia ya ushabiki wa   kisiasa usio kuwa na tija  badala yake  kushirikiana  na viongozi waliopo  madarakani   ili kuleta maendeleo nchini.
Amesema  viongozi wana nafasi kubwa ya kutoa mchango wao katika kuwaelimisha wananchi juu ya mambo mbalimbali ya maendeleo  kwani upinzani sio chuki na  kuwataka  viongozi kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu ya uraia hasa kwa  vijana.
Hata hivyo Juma Ali Khatibu amewataka viongozi kukumbuka na kuwacha kujisahau wakati wanapochaguliwa  kupewa  madaraka ya uongozi na wananchi kwani bila ya kuchaguliwa na kuaminiwa wasingekuwa na vyeo walivyonavyo hivi sasa.
Aidha ametoa wito kwa  baadhi  ya viongozi wanaoshindwa kutimiza majukumu yao kwa wananchi waliowachagua kuwajibika ipasavyo kwani wao ni watetezi hasa kwa wananchi wanyonge kusikiliza vilio na changamoto zinazowakabili wananchi.
chanzo:Zanzibar24 

Comments