Kamati ya kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu na kitaifa yataka kuona matokeo ya fursa za masoko katika jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Kamati ya kusimamia  Ofisi za Viongozi  wakuu na kitaifa  kwa  mwaka wa fedha  2017/2018  imeishauri  idara ya mipango,sera na utafiti  kuhakikisha kuwa  kunakuwa  na matokeo  ya utafiti  kwa wananchi  juu ya fursa za masoko  katika jumuiya  ya Afrika ya Mashariki.
Akiwasilisha ripoti   hiyo  ya kamati  katika  kikao  cha baraza la wawakilishi  Mwenyekiti wa kamati ya kusimami  ofisi za viongozi  wakuu wa kitaifa Omar Seif Abeid amesema  pia idara lazima  iwe inatoa taarifa za mpango  wa  kupunguza  umaskini  ili jamii iweze kuelewa hatua zinazochukuliwa  na serikali katika  kuondoa umaskini  nchni.
Wakati huo  huo Mwenyekiti  huyo wa kamati ya kusimamia Ofisi za viongozi amezungumzia   changamoto zinazoikabili tume ya kitaifa  ya uratibu na udhibiti dawa za kulevya  nchini ambapo amezitaja miongoni mwa changamoto hizo ni upotevu wa vielelezo vya kesi  na kukosekana  kwa takwimu  halisi  juu ya idadi ya vijana walioingia na kutoka  katika  vituo vya tiba  na Marekebisho ya tabia sober house.
Baada ya  kugudnua  changamoto hizo Kamati hiyo imetoa ushauri kwa tume ya uratibu na udhibiti wa dawa za kulevya  kuwa karibu na taasisi zote zinazohusika  na kesi za madawa ya kulevya ili kuhakikisha kwamba wale wote wanaojishughulisha  na biashara  haramu  ya dawa za kulevya  wanachukuliwa hatua za kisheria na kwamba  tatizo la  upotevu wa vielelezo vya  kesi hizo halitokei tena kama hapo awali.

Comments