elevisheni ya CNN ya Marekani imetangaza
habari hiyo na kufafanua kuwa, mfumo wa Marekani wa kujilinda na
mashambulizi ya makombora unaojulikana kwa jina la SM-3 ulifanyiwa
majaribio jana kwa kufyatua kombora katika jimbo la Hawaii, hata hivyo
kombora hilo limeshindwa kupiga shabaha iliyokusudiwa.
Duru za CNN zimesema kuwa, Wizara ya
Ulinzi vya Marekani ilificha kufeli huko kutokana na hali ya wasiwasi
iliyopo hivi sasa baina ya nchi hiyo na Korea Kaskazini.
Huko nyuma makombora ya Marekani
yalikuwa yakifyatuliwa kutoka katika manuwari za kivita, lakini mara hii
kombora hilo limefyatuliwa kutoka nchi kavu na kufeli.
Ikumbukwe kuwa
Japan ndiyo iliyokuwa inatarajiwa kununua mfumo huo wa Marekani wa
kujilinda na mashambulizi ya makombora.
Mzozo baina ya Marekani na Korea
Kaskazini umechachamaa zaidi katika miezi ya hivi karibuni kiasi kwamba
majeshi ya nchi hizo mbili yamewekwa katika hali ya tahadhari hususan
sehemu ambazo kuna hatari ya kushambuliwa kwa makombora.
Mara kwa mara Pyongyang imekuwa
ikitishia kuishambulia Marekani kwa silaha za nyuklia hasa kila pale
rais wa nchi hiyo Donald Trump anapopayuka na kutoa maneno ya kichochezi
dhidi ya Korea Kaskazini.
chanzo:parstoday.
Comments