Iran yajibu tuhuma za Marekani: Siasa zenu ndio chanzo hasa cha kuvurugika uthabiti Mashariki ya Kati.
Taarifa iliyotolewa na ofisi ya uwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa imebainisha kuwa: wakati ukweli halisi wa mambo unaonyesha kuwa Iran imekuwa ikifanya jithada za dhati za kuondoa mivutano nchini Syria, serikali ya Marekani ndiyo inayokwamisha kila jitihada zinazofanywa kuhusiana na suala hilo.
Mbali na taarifa hiyo kusisitiza kwamba mchango na nafasi ya Marekani katika kuliimarisha kundi la kitakfiri la Daesh na ugaidi katika eneo haiwezi kukanushika, imebainisha kuwa chokochoko na uingiliaji wa kinyume cha sheria unaofanywa na Marekani katika nchi mbalimbali hususan, Iraq, Libya, Syria, Lebanon na Afghanistan umevuruga uthabiti katika nchi hizo na kulisababishia eneo maafa na masaibu.
Haley ametoa matamshi hayo dhidi ya Iran kufuatia kutunguliwa na kuangushwa na jeshi la Syria ndege ya kivita ya Israel iliyovamia anga ya nchi hiyo.
Kuangushwa ndege hiyo ya kivita ya utawala vamizi wa Israel kumeukasirisha utawala huyo haramu na muungaji mkono wake wa jadi Marekani.
chanzo:parstoday.
Comments