Asimulia alivyopigwa na kunusurika kuripuliwa moto na mumewe Unguja.

Related image
Mwanamme mmoja alietambulika kwajina la Is-haka Ibrahim Abdallah mwenye umri wa miaka 36 amshushia kipigo kizito mkewe na kummwagia mafuta yataa kwa lengo la kumripua na hatimae  kukimbilia nyumbani kwa sheha na kupata msaada.

Tukio hilo limetokea saa moja na nusu usiku huko Kibweni Wilaya ya Magharib A Unguja.

Majeruhi huyo akielezakwa masikitiko  mkasa huo ulivyotokea amesema “kuwa nilikua namuaga kuwa naendazangu nyumbani kwa hali yangu akainuka na kuanza kunipiga na akachukua kisu akataka kunichania nguo amenipiga na kuniumiza na aliniambia anataka kunichoma kisu pia aliniambia atakaponikuta popote atanipiga amenipiga nimevimba mwilini amenichuna na baada ya hapo alikuja na mafuta ya taa akanimwagia ili anichome moto”

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Sheha wa Shehia  ya Kibweni Subira Haji Yahya anaeleza mkasa huo “kesi hii imetokea kweli mama huyo amekuja nyumbani mwangu nakilio na nguo zake zime chanika sehemu za mwili zilikua zipo wazi nayeye alipokuja alisema kweli alikua anataka kumchoma moto”

Hadi sasa kesi hiyo imeshafikishwa Kituo cha Polisi Bububu.

chanzo: zanzibar24.

Comments