Akizungumza
na wananchi wa kisiwapanza marabaada ya kutembelea maeneo mbali mbali yakiwemo
ya kilimo yaliyo athiriwa na maji chunvi ikiwa ni miongoni mwa jitihada za
jumuiya hiyo kutoa elimu ya mazingira Nd. Marzouk amesema licha ya juhudi mbali
mbali zinazo chukuliwa namashirika binafsi,
NGOs, na taasisi za Serekali lakini bado athar za mabadiliko ya tabia nchi
zinaendelea kuathiri wananchi wa kisiwa hicho.
Amesema
suala la uhifahdi wa mazingira nijukumu la kila mtu na sio taasisi moja tu,
hivyo amewataka wananchi kupanda miti kwa wingi ili kuzuiya maji ya bahari
yasivamie maeneo yakilimo.
Aidha
Nd. MARZOUK amesema kitu cha msingi katika kuthibiti hali hiyo isiendelee ni kupanda
miti ya mikandaa katika maeneo ya bahari, ili kuzuiya kasi ya maji kuingia
mashambani.
Nae
Mwajuma Ali Hassan ambae ni mkaazi wa Kisiwapanza amesema suala la ukataji wa
miti ovyo limewaathiri sana wakulima kutokana na maeneo ya kilimo kuvamiwa na
maji chunvi, ambapo zaidi ya eneo lenye ukubwa wa hekta 200 maeneo ya kilimo na
makaazi ya wananchi yamesha athiriwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
Comments