Malezi ya pamoja ni muhimu kwa kizazi cha sasa na baadae.

Image result for smzJamii imeshauriwa kurejesha malezi ya pamoja ili kulinda maandili yasiendelee kuporomoka siku hadi siku.

Akizungumza katika kikao cha wazee pamoja na mashekhe wa mji wa Tumbe Sheha wa Shehia ya Tumbe Mashariki Nd. Seif Omar Khamis amesem kwa sasa maadili yamepotea hivyo ipo haja jamii kuungana ili yasizidi kudidimia.

Amesema bilaya mashirikiano ya pamoja hakuna jambo lolote ambalo litaloleta matunda na mwisho wake nikuzaa kizazi kilicho kosa maadili mema.

amefahamisha kuwa kukithiri kwa wizi ma mazao, mifugo na hata vitendo vya udhalilishaji vimechangiwa kwa asilimia kubwa na ukosefu wa maadili ndani ya jamii.

Aidha ameitaka jamii ya watu wa Tumbe kupitia mashekhe kuendelea kuelimishana juu ya vitendo vya udhalilishaji ikiwemo liwati kwani vitendo hivyo vinaikosesha hadhi na heshma  jamii yao.

Kwaupande wake Sheha wa Sheia ya Tumbe Magharibi Nd. Masoud Khamis amesema Tumbe imejaaliwa kuwa na rasilimali nyingi ikiwemo Mmikorosho na Mikoko hivyo nivyema kuzitumilia ipasavyo bila kuathiri mazingira hatimae kusababisha majangwa.

Akizungumzia kuhusu wizi wa mifugo Sheha huyo amesema kwa sasa wanajiandaa kuunda sheria ndogo ndogo zitakazo wasaidia kupambana na wale wote watakao jari kufanya vitendo hivyo.


Nae mmoja ya waulamaa wa mji wa Tumbe Utasdh Juma Abdurrahman Juma aesema lazima jamii ijuwe kuwa Allah ( SW ) ametuleta duniani kwa ajili ya kumuabudu nasivyenginevyo hivyo nivyema kurejea kwake pale tulipo kosea ili aweze kutusamehe.

Comments