Kisiwa cha Fundo Pemba kunufaida na umeme.

Image result for katibu mkuu wizara ya Maji Nishati na Mazingira zanzibarKatibu Mkuu wizara ya Maji Nishati na Mazingira Mh. Ali Khalil Minza amsema wakati umefika sasa kwa wananchi wa kisiwa cha fundo kuwendelea kuapata nishati ya umeme itayo wasaidia katika matumizi yao yakila siku.

Akizungumza na waandishi wa habari huko katika ukumbi wa  taasisis ya nyaraka na kumbu kumbu za Serekali chake chake ikiwa ni shamra shamra za kutimiza miaka 54 ya Mapinduzi Zanizbar amesema azma ya serekali ni kuwafikishia wananchi wake huduma ya umeme hadi vijijini na sasa lengo hilo naendelea kutekelezwa.

Amesema kwa kutimiza ahadi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Ali Mohd Shein alitoa kwawananchi wa kisiwa cha fundo kupatiwa umeme sasa imekamilika.


 amefahamisha kuwa serekali ya Mapinduzi Zanzibar imefanya jitihada kubwa ya kupeleka umeme fundo kwa kupitia wataalamu wa ndani na wamefanikiwa kulaza waya chini ya bahari wewenye kiwango cha WALT. 1.7 kwa urefu wa km 2.4.

Amefafanua kuwa azma ya serekali ni kuwafikishia wananchi wa visiwa vya unguja na pemba huduma ya umeme kwa haraka zaidi.


Jumla ya wananchi 352 wa kisiwa cha fundo  wameshaunganishiwa huduma hiyo kati ya wakaazi elfu 3000 waishio kisiwani humo.

Comments